Photo Gallery

  • Watumishi wa sekta ya maji

    Naibu waziri wa sekta ya maji Mhe Mhandisi Kundo Mathew amewapongeza watumishi wa sekta ya maji mkoani Morogoro kwa kufanya kazi kwa bidii na kuifanya sekta hiyo kuwa ni msaada wa upatikanaji wa maji safi na salama kwa wananchi wa mkoa wa Morogoro. Ameyasema hayo katika kikao baina yake na watumishi wa sekta ya maji mkoa wa Morogoro kilichofanyika leo 25/05/2024 katika ukumbi wa hoteli ya Morena. Mhe. Kundo amewaasa watumishi kupendana na kutojihusisha na majungu katika kazi kwani vitendo hivyo vinashusha ufanisi wa kazi katika Wizara. Pia amewasisitiza watumishi wa sekta hiyo kufanya kazi kwa kushirikiana kwani mafanikio ya sekta ya maji hayaletwi na mtu mmoja Pamoja na hayo Mhe. Kundo amewashukuru watumishi wa sekta ya maji kwa kumpokea vizuri katika wizara hiyo na kuahidi ushirikiano wa hali na mali katika kuhakikisha wizara ya maji inakuwa ni mfano bora kiutendaji katika utoaji huduma bora kwa wananchi wa Tanzania. Ikumbukwe kuwa siyo muda mrefu tangu Mha. Kundo ateuliwe na Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan kuwa Naibu Waziri wa Maji chini ya waziri wake Mhe. Jumaa Aweso. Kikao hicho kilihusisha watumishi walio chini ya sekta ya maji katika mkoa wa Morogoro kutoka taasisi za MORUWASA, BODI YA MAJI-BONDE LA WAMI RUVU, RUWASA, IFAUWASA, GAUWASA, TURUWASA na Maabara ya Ubora wa Maji.

    .

    Posted On : May, 20,2024

  • EWURA

    MORUWASA imetembelewa na wawakilishi kutoka EWURA Kanda ya Kati ambao wamefika kwa lengo la kutekeleza majukumu yao ya kiudhibiti katika Mamlaka yetu ikiwa ni pamoja na kukagua utekelezaji wa majukumu yetu.

    .

    Posted On : May, 20,2024

  • EWURA CCC YAPONGEZA MIKAKATI YA MORUWASA.

    Baraza la Ushauri la Watumiaji wa Huduma za Nishati na Maji ( EWURA CCC) limepongeza mikakati na miradi inayotekelezwa na MORUWASA ya kuhakikisha changamoto ya maji Morogoro inamalizika

    Pongezi hizo zimetolewa Juni 8,2023 na Kaimu Katibu Mtendaji wa EWURA CCC Bi. Stella Lupimo wakati wa ziara ya Bodi na Wajumbe wa baraza hilo ya kutembelea na kujifunza shughuli zinazotekelezwa na Mamlaka ya Majisafi na Usafi wa Mazingira Morogoro (MORUWASA)

    Bi. Lupimo amesema wamejionea namna MORUWASA ilivyojipanga katika kutatua changamoto ya maji Morogoro. "Moja ya vitu ambavyo tumejifunza na tumeondoka navyo kama baraza ni kwamba MORUWASA wamejipanga"

    Naye, Mkurugenzi Mtendaji wa MORUWASA Mha. Tamim Katakweba amesema kukamilika kwa miradi mbalimbali ya muda mfupi na kati inayoendelea kutekelezwa itapelekea Manispaa ya Morogoro kuwa na uhakika wa huduma ya maji kwa zaidi ya asilimia 100.

    .

    Posted On : Juni, 08,2023

  • Ofisi ya maji taka na mazingira.

    Zoezi la Usafishaji vyanzo vya maji vya vituli namwanzomgumu, uhamasishaji wa wananchi wanaoishi karibu na vyanzo hivyo kutunza mazingira, kutofanya shughuli za binadamu kwenye vyanzo vyanzo vya maji kama kufulia mtoni moja kwa moja,kuelekeza namna bora ujenzi wa vyoo ili visichafue vyanzo vya maji pamoja na kilimo bora ambacho ni rafiki wautunzaji wa ubora wa maji .

    Posted On : March, 23,2020

  • Ofisi ya maji taka na mazingira

    Zoezi la Usafishaji vyanzo vya maji na utoaji elimu kwa wananchi namna bora ya utunzaji vyanzo hivyo likiendelea baadhi ya maeneo ya mkoa wet

    Posted On : March,24,2020.

  • Zoezi la ufuatiliaji bili kwa wateja

    Baadhi ya watumishi wakiwa pamoja katika zoezi la ufuatiliaji bili za maji kwa wateja

    Posted On : March,20,2020

  • Ziara ya katibu mkuu wizara ya maji

    Katibu mkuu akiwa na badhi ya watendaji wa MORUWASA wakati wa ziara yake alipotembele maeneo tafauti kuangalia miradi ya maji inayo endelea

    Posted On : .....